Friday, February 18, 2011

Wakuu wa nchi walipotembelea eneo la maafa

 Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilali akitembelea kwenye kambi ya jeshi la wananchi eneo la Gongolamboto ambapo milipuko ya mabomu ilitokea na kusababisha vifo vya watu na uharibifu wa nyumba na mali. 
Amiri jeshi mkuu na Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania akiongea na wanahabari baada ya kutembelea eneo lililopatwa na maafa ya kulipukiwa na mabomu huko Gongolamboto jana
Waziri wa Ulinzi Dk. Hussein Mwinyi akizungumza na Makamanda wa jeshi la ulinzi wakiongozwa na mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange (wa pili Kulia)


                             
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Hussein Mwinyi akiongea na makamanda wa JWTZ katika kambi ya Jeshi la Wananchi Gongolamboto mara baada ya kutembelea kazi hiyo baada ya milipuko ya mabomu.

Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda akipata maelezo ya madhara ya mabomu yaliyolipuka kwenye kambi ya jeshi ya Gongolamboto alipotembelea.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais (Sera na Bunge) Mh William Lukuvi ( mwenye suti nyeusi) na Spika wa Bunge Mama Anne Makinda (watatu kulia) wakitoa salamu zao baada ya kutembelea eneo la maafa huko Gongolamboto.

No comments:

Post a Comment